Monday, 26 August 2013

HUU NDO MWONEKANO WA HEMEDY PHD BAADA YA KUPATA AJALI....AKIWA NA BANDAGE USONI LAKINI HERENI BADO HAJATOA


Muigizaji Hemedy Suleiman ambaye pia ni mwanamuziki wa Bongofleva amefunguka kuwa anaendelea vizuri baada ya kupata ajali mbaya ya gari na gari hilo kudaiwa kuharibika. Hemedy alikuwa akimsindikiza Gerry Wa Rhymes ambaye pia ni msanii 
maarufu nyumbani kwake Sinza na kupata ajali baada ya kugonga kalivati. Kupitia mtandao mmoja wa kijamii Hemedy ameandika "Namshukuru mungu naendelea vizuri baada ya kupata ajali mbaya iliyonikuta..ahsanteni kwa dua zenu, kifua tu ndiyo kimeumia na mkono" 
Get well soon Hemedy 

No comments:

Post a Comment