Mwanaume ambae alikua akichunguzwa na askari wa Norwegian kuhusu uvamizi wa Mall ya westage iliyopo nchini Kenya ni Hassan Abdi Dhuhulow
Kijana huyo wa Norwegian ambae ni raia wa Somalia anaisiwa kwamba ameshiriki kwenye mipango yote mpaka kufanikisha uvamizi huo.....
BBC imezungumza na ndugu yake anaeishi Norway ambae amesema kwamba kijana huyo aliondoka mjini Larvik na kwenda Somalia mnamo mwaka 2009
Wiki iliopita Mkuu wa upelelezi wa Norway alituma vijana wake nchini kenya kuhakikisha ripoti kwamba raia wa Norwegian anausika kwenye uvamizi wa Mall io ambao ulitokea mnamo tarehe 21 mwezi wa Tisa ambao uvamizi huo ulidumu kwa siku 4 mfululizo
Mpaka sasa Bado aijafahamika ni magaidi wangapi walikuemo kwenye uvamizi huo Lakini askari walikisia kwamba walikuepo magaidi 10-15 lakini CCTV camera ilirekodi baadhi ya video na uongozi wa kenya ulitoa video hizo na cha kushangaza ni kwamba ni Magaidi wanne tu ndo walioonekana kwenye video hizo huku Hassan Abdi Dhuhulow anasadikiwa kuwa ni mmoja kati ya wale wanne
Hassan Abdi Dhuhulow amezaliwa Somalia lakini yeye na familia yake walienda nchini Norway mnamo mwaka 1999 kama wakimbizi
Baada ya kusema kwamba Dhuhulow ameonekana kwenye CCTV basi ndugu yake huyo alisema kwamba yeye ajui na kama ndo yeye atakua ameshawishiwa basi
Mwandishi wa Habari Gabriel alisafiri mpaka mjini Larvik kilomita 120 kusini mwa Oslo, ambapo familia ya Dhuhulow walikua wakiishi
Morten Henrisksen mmoja wa majirani wa familia ya Dhuhulow amesema yakwamba ajaonana na Dhuhulow kwa miaka mingi lakini alikua kijana mzuri na pia hakupenda maisha ya Norway alikua akiingia kwenye majibizano na kupigana, baba yake alikua na mashaka nae sana....Mr Henriksen alisema hayo
Baada ya yeye kuangalia video io alisema kwamba ''yule alievaa shati jeusi anaweza akawa Dhuhulow''
0 comments :
Post a Comment