Taarifa ambazo zimenifikia ni kwamba wale watuhumiwa wa ugaidi waliokamatwa wakifanya mazoezi msituni 88.4 Mtwara, walipelekwa Mahakamani asubuhi ya leo October 17 2013 lakini kutokana na baadhi ya taratibu za kimahakama ikashindikana kupandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Wilaya ya Mtwara hivyo wakarudishwa mahabusu mpaka hapo itakapoamuliwa ni siku gani wapelekwe tena Mahakamani.
Mwanzoni walikua wamekamatwa 11 tu lakini taarifa nyingine zilizoifikia millardayo.com zinaamplfy kwamba idadi imeongezeka baada ya wengine wawili kukamatwa kulekule walikokamatiwa wengine ambapo hawa wawili hawakukutwa na silaha wala kingine chochote kama ilivyotokea kwa wale wa mwanzo ambao walikutwa na mapanga, silaha mbalimbali pamoja na CD za DVD ambazo zinamafunzo ya kijeshi ya Al Shabaab na Al Qaeda.
Wawili hawa wamekiri kwamba mwalimu wao kule msituni alikua akiwapa mafunzo ya aina mbalimbali ikiwemo kupiga karate, utumiaji wa silaha ambapo pia walikua wakiishi hukohuko msituni kwenye Mapango.
Hili hapa juu ndio gari lililobeba baadhi ya hao Watuhumiwa wa ugaidi.
0 comments :
Post a Comment