Wednesday, 20 November 2013

RONALDO APIGA HATRICK,IBRAHIMOVICH APIGA MBILI LAKINI URENO YAFUZU KOMBE LA DUNIA

ronado_7a41e.jpg
Mabao matatu yaliyopigwa na Cristiano Ronaldo yameivusha Ureno kucheza Kombe la Dunia mwakani. Ushindi huo wa mabao 3-2 dhidi ya wenyeji Sweden ambao nao mabao yao mawili yalifungwa na nahodha, Zlatan Ibrahimovic. Katika mechi ya kwanza, Sweden ikiwa ugenini ilikutana na kipigo cha bao 1-0. Ureno ilianza kupata bao kupitia Ronaldo, wenyeji Sweden wakasawazisha na kufunga mabao mawili kupitia Ibrahimovic. Lakini Ronaldo alipiga mabao mawili harakaharaka na kumaliza kabisa matumaini ya wenyeji.

No comments:

Post a Comment