.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

Bomoa Bomoa,Tinga Tinga 3 Zatua Bonde La Msimbazi

Tinga Tinga likibomoa katika eneo la Mkwajuni jijini Dares salaam.
Tinga tinga takribani tatu zipo katika Bonde la Mto msimbazi katika eneo la Mkwajuni jijini Dar es salaam zikiendelea na kazi ya kubomoa nyumba zilizojengwa katika eneo hilo.
Bonde la Mto msimbazi ni moja ya eneo linalodaiwa kuwa hatarishi kufuatia kujaa maji  ambayo yamekuwa yakisababisha  vifo vya watu hasa katika msimu wa mvua.
Kwa upande wake  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi mwishoni mwa mwaka jana alitoa siku 14 kwa wakazi wote wa mabondeni kuondoka kabla serikali haijachukua hatua kali ikiwemo kubomoa nyumba hizo.
Aidha, siku ya 14 leo tarehe 5 ndiyo mwisho ambayo serikali imeanza kwa kasi kubomoa nyumba  zilizojengwa katika maeneo hatarishi.
Kwa upande wa baadhi ya wananchi katika Bonge la Mkwajuni wameiomba serikali kuwapatia muda katika maeneo hayo hatarishi  ili wajipange  kutimiza maagizo hayo ya serikali yanayowataka kuhama haraka iwezekanavyo.

Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad