.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

IJUE SIKU YA MABLOGGERS DUNIANI

Ikiwa zipo siku za akina mama, za akina nanihii na nanihii sijui kina nani vile, kwanini nasi tusiwe na yetu? Pengine hili ndilo swali ambalo Bw. Nir Ofir, alichojiuliza na baada ya kuchanganya na ubunifu wake kidogo, basi akaibuka na wazo kuwa Agosti 31 inafaa kuwa Siku ya Blogi Duniani, kwa maana ukiamua kuingiza usanifu wa maandishi katika tarakimu 3108, zinaweza kusomeka Blog.
Leo ni Siku ya Blogi/Kublogi/Mabloga, duniani, ikiwa ni mwaka wa pili kwa siku hii kuadhimishwa. Kwa wale ambao hawajabahatika kujua nini maana ya siku hii, wanaweza kusoma hapa maana ya siku hiyo kama ilivyotafsiriwa na mwanaharakati Maitha anayemiliki blogi ya Bangaiza.
Kwa wale ambao hawakubahatika kushiriki mwaka jana, pengine itakuwa vyema wakatambua ushiriki wa wenzao, wakiwemo Watanzania kadhaa walioshiriki siku hiyo ikiwa ni pamoja na Bw. Ndesanjo Macha, ambaye katika siku hiyo aliandika makala unazoweza kuzisoma kwa kubofya hapa na hapa, na makala hiyo ikavutia watu wengi kuichangia. Soma maoni ya waliochangia makala hiyo kwa kubofya hapa.
Mwingine alikuwa kaka yangu Jeff Msangi, wa harakati, ambaye aliandika makala hii, kuhusiana na siku ya kublogi duniani, na vilevile hata mimi mwenyewe kupitia Blogi yangu nilishiriki kwa kuandika makala unayoweza kuisoma kwa kubofya hapa, na Bw. Akiey ambaye ni mmoja kati ya niliowagusia siku hiyo alinitumia ujumbe nilioufurahia kwahakika.
Kwa namna ya kipekee nitaomba ushiriki wangu wa mwaka huu uhusishe kuwatambua watu kadhaa kutokana na sababu mbalimbali nikianza na ndugu yangu, mwanaharakati, mbunifu na kinara wa mabadiliko katika blogi za Watanzania. Na hapa namaanisha ndugu yangu MK mwenye kumiliki blogi ya Vijimamboz.
Kwa wale ambao wamekuwa wasomaji wetu, nadhani watagundua kuwa blogi zetu nyingi zimekuwa na mabadiliko ya kimwonekano zikawa na sura ya kuvutia zaidi. Hii ni kazi ya huyu mheshimiwa ambaye amekuwa yuko tayari kutoa msaada wa namna yoyote ile kwa yeyote anayejihisi ana tatizo katika kusukuma gurudumu la kublogi duniani.
Ameshafanya kazi kadhaa zikiwemo za kuleta viungo kwa ajili ya kuwezesha mambo mbalimbali kwenda kwa urahisi na kwa namna ya kupendeza, amenishawishi nami nikajiingiza katika ujenzi (ona jumba nililolijenga hapa), lakini zaidi ya yote yuko huru kumsaidia mtu kwa lolote lile. Kwa wale wenye kuwa na maswali mbalimbali kuhusu ku-blogi, wanaweza kumtembelea katika blogi yake kwa kubofya hapa.
Ninaye mwana-Blogi mwingine ambaye kazi zake ukizisoma zinaweza kukufanya ujiulize mara kadhaa, hivi kwanini watu wa namna hii hawapewi nafasi za kuongoza nchi, na hapa namzungumzia dada yangu Hawra Shamte. Unaweza kuona kile anachokiandika ambacho kinanivutia kwa kutembelea blogi yake ya Mnyonge Mnyongeni.
Ukiachilia mbali ndugu zangu weeeeengi ambao nimekuwa nikiwazungumzia mara nyingi kama Ndesanjo, Reginald, Jeff nakadhalika kuna Watanzania wengine ambao kwa hakika nitapenda kutambua kuwepo kwao katika siku hii ikiwa ni pamoja na jamaa zangu wa Kijijini (Ulaya kuna Vijiji?) ambao unaweza kuwapata kwa kuingia hapa.
Na….oh!! Nitamsahau dadangu na mpishi wetu Miriam? Hapana, mchango wako ni mkubwa sana dada, tumekuwa tukitangaza lugha, tumekuwa tukitangaza amani tuliyonayo, utulivu na kila kitu, lakini ni nani aliyekumbuka kuwa hata mapishi ya Kitanzania ni muhimu yakatangazwa kwa kuwa ni ya aina yake kama sio wewe? Kwa wasio au wanaotatizwa kiasi na namna ya kukorofisha masuala ya jikoni nadhani mkitembelea hapa, mtakutana na mtaalamu wa mapishi, dada Miriam.
Na kwa wale ambao wamekuwa na imani sawa na ile ya Ndesanjo, kuwa baadhi ya nyakati ni vyema kuwasikiliza wenye kukuponda zaidi kuliko wale wanaokuunga mkono kwa kila hoja, nadhani itakuwa vyema nikiwaambia kuwa ushiriki wangu katika siku hii ya kublogi duniani, utahusisha pia kutambua uwepo wa blogi inayozungumzia filamu ambayo imekuwa gumzo kubwa nchini Tanzania, namaanisha filamu ya Darwins Nightmare iliyotengenezwa na Bw. Hubert Sauper. Unaweza kuitembelea (na ukaiona vipande vipande filamu yenyewe) kwa kubofya hapa, na kasha ukashiriki mjadala kuhusu filamu hiyo kama unavyoendelea kwa Wanakijiji wa Tanzania walioko Ulaya, walau ukiwa unajua jambo kuihusu.
Wapo wengi ambao natambua mchango wao kwa ujumla, na ni wazi kuwa siwezi kuwataja wote, kwa maana hiyo naomba niwaeleze kuwa kwa ujumla wenu natambua mchango, ushiriki na umuhimu wenu katika kazi hii tuliyoamua kuifanya. Yapo mambo kadhaa ambayo tutatakiwa kuyajadili kwa kina hasa kwetu sisi tulio Watanzania, na naamini wapo ambao wataongoza mijadala hiyo kulingana na jinsi tutavyojipanga nikiamini kuwa mwaka ujao kwa wale tutaobahatika bilashaka tutakuwa na mengi ya kuzungumza katika siku kama hii.
Unaweza kupata taarifa zaidi kuhusu siku hii kwa kuingia hapa au hapa
KILA LAKHERI WANA-BLOGI WOTE KATIKA SIKU HII
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad