.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

SIMBA YAMTEMA HUMOUD NA CHANONGO



SIMBA imeondoka jana Jumatatu kwenda Tanga kuikabili Coastal Union kesho Jumatano lakini imechomoka kwa basi ikiwa na wachezaji 22 tayari kwa mchezo huo ikiwaacha Haorun Chanongo, Abdulhalim Humoud, Betram Mwombeki, Ramadhan Chombo ‘Redondo’ na Henry Joseph.
Wekundu hao wataivaa Coastal Union ambayo jana Jumatatu ilitangaza kumtema kocha wake, Hemed Moroco na kumpa timu, Joseph Lazaro.
Habari ambazo  Mwanaspoti imepata zinasema kuwa Humoud na Chanongo wameachwa kutokana na kucheza chini ya kiwango katika mchezo dhidi ya Yanga juzi Jumapili na timu hizo kutoka sare ya mabao 3-3.
Wachezaji hao walitolewa kipindi cha pili na nafasi zao kuchukuliwa na William Lucian na Said Ndemla waliobadilisha mchezo na kuifanya timu yao iliyokuwa nyuma kwa mabao matatu kusawazisha yote na matokeo kuwa sare.
Hata hivyo baada ya mchezo huo Kocha Abdallah Kibadeni alilalamikia hujuma na kudai kuna baadhi ya wachezaji walitumiwa na baadhi ya watu walioivamia kambi ya timu hiyo ili wacheze chini ya kiwango.
“Kuna watu walikuja kambini na kuwapandikiza maneno wachezaji, na waliopandikizwa maneno hawakucheza  vile inavyopaswa kipindi cha kwanza na wakaruhusu mabao matatu ya haraka, siwezi kuwataja kwa majina watajijua na kujichuja wenyewe, yule Humoud nilimpanga makusudi kama mlivyoona ndio maana nikamtoa,” alisema Kibadeni.
Wachezaji wengine kama Mwombeki hajaungana na wenzake safarini kwa sababu ana kadi tatu za njano zinazomzuia kucheza mchezo huo wakati Henry Joseph bado anaendelea kutumikia adhabu baada ya kutofautiana na kocha na Ramadhan Chombo ‘Redondo’ amepelekwa timu B.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad