.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

STEPHEN WASIRA AFUNGUKA KUHUSU KUMPANGIA RAISI WAGENI

*Asema hampangii Rais nani aonane naye
*Mtikisiko mkubwa watarajiwa bungeni Dodoma
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wasira, amesema hana mamlaka ya kumchangulia Rais nani akutane naye.

Alitoa kauli hiyo katika mahojiano na Rai yaliyofanyika Jumanne wiki hii ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam kuhusu hali ya siasa nchini katika kipindi ambacho umma wa Watanzania unasubiri kusainiwa kwa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete.

“Taarifa kwamba naweza kumwambia Rais Kikwete aonane na huyu au asionane na yule si za kweli, Rais ana mamlaka yake, ana ofisi yake binafsi, pia yeye ni kama baba hivyo mtu yoyote bila kujali itikadi ana haki ya kuonana na Rais.


“Ninachofahamu muswada ukija Rais atasaini kwa sababu taratibu na kanuni zote zimefuatwa, lakini kama wenzetu wanahitaji kumuona Rais ni sawa, na amesikia wito na amekubali. Tusubiri matokeo ya mazungumzo,” alisema.

-Mtanzania
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad