.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

KASEJA WAPIGA BAO TAMU

 
KIPA mpya wa Yanga, Juma Kaseja, ameandika rekodi nyingi na tofauti akiwa na klabu yake ya zamani ya Simba kwenye Ligi Kuu Bara na sasa Kelvin Mhagama amemuonya Ally Mustapha ‘Barthez’ wa Jangwani.
Rekodi ya kwanza ya Kaseja ni kuipa Simba taji la ubingwa wa Ligi Kuu bila ya kupoteza mchezo hata mmoja. Hiyo ilikuwa msimu wa 2011/12.
Pia ana rekodi ya kucheza dakika 2,340 ambazo ni sawa na michezo 26 ya ligi nzima ya Bongo bila kufanyiwa mabadiliko na kocha wake wala kuwa kwenye adhabu ya kadi au kuumia na kukosa mchezo.
Achilia mbali rekodi hizo, msimu huo huo wa 2011/12, Kaseja akiwa na Simba alidaka dakika zote 1,170 ambazo ni sawa na mechi 13 za mzunguko wa kwanza wa ligi bila kufanyiwa mabadiliko.
Utafiti uliofanywa na Mwanaspoti baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu kumalizika na kuzungumza na mabenchi ya ufundi ya timu 14 zinazoshiriki Ligi Kuu hakuna kipa ambaye ameweza kufikia rekodi hiyo mpaka sasa.
Kipa wa Coastal Union ya Tanga, Shabaan Kado, alijaribu na kutaka kumfikia Kaseja lakini ghafla alijikuta akiteleza na kuishia njiani.
Akizungumza na Mwanaspoti, Kado alisema: “Nimecheza mechi zote 13 kwenye ligi ingawa kuna moja nilishindwa kuimaliza kutokana na kuumia, nilidaka kwa dakika 45 za kwanza lakini nikashindwa kuendelea hivyo Rubawa (Said) alichukua nafasi yangu.”
Katika hatua nyingine, kipa wa zamani wa Simba, Kelvin Mhagama,  amesema kama angekuwa yeye ndiye ‘Barthez’ angeondoka Yanga na kurudi Simba wala asingeremba kwa vile uwezekano wa kipa huyo kucheza kikosi cha kwanza Yanga kuanzia sasa ni finyu.
Kipa huyo mkongwe alisema ukitaka kuona uhondo wa makipa hao ni lazima Barthez arudi zake Simba na ndio upinzani wao utaonekana kwa kuwa yeye anaamini uwezo wao upo sawa.
Akizungumza na Mwanaspoti mjini Dodoma, Mhagama alisema ujio wa Juma Kaseja ndani ya Yanga ni kama kikosi hicho kukosa imani na Barthez hasa baada ya sare mabao 3-3 na Simba, hivyo nafasi yake ndani ya timu hiyo ni ndogo.
Mhagama alisema hakuamini kama Kaseja anaweza kusajiliwa Yanga kwa kuwa aliamini uwezo wa Barthez na Dida ndani ya kikosi hicho ni mkubwa hivyo kutohitajika kipa mwingine zaidi ya hao.
“Uwezo wao hasa Kaseja na Barthez unafanana, Yanga wamekosa imani na Barthez, kwa uzoefu wangu namsihi dogo afungashe virago vyake kama vipi arudi zake Simba pale atapata nafasi maana hamna kipa, huyo Dhaira (Abel) ni bure tu najua watampokea tu, lakini akibaki Yanga atasugua benchi tu,”alisema Mhagama ambaye naye aliwahi kucheza Simba akiwa na Kaseja, lakini akashindwa vita ya kuwania namba kikosi cha kwanza.
CHANZO:MWANASPOTI
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad