Mwili wa jambazi hilo |
Kijana
mmoja ambaye hajatambulika jina lake mwenye umri kati ya miaka 26 hadi
30 ameuawa kwa kupigwa risasi wakati akiwa na wenzake wakijaribu kuvunja
duka maeneo ya Shunu, kata ya Nyahanga wilayani Kahama mkoani
Shinyanga.Tukio
hilo limetokea majira ya saa nane usiku wa kuamkia leo ambapo jambazi
hilo likiwa na wenzake watatu liliuawa kwa kupigwa risasi kichwani na
Wilson Masolwa (63) mkazi wa mtaa huo ambaye alijeruhiwa kwa mapanga.
Mtu
huyo ameuawa kwa Bunduki aina ya Shortgun ambayo hata hivyo wenzake
waliipora baada ya kumkata mapanga Masolwa na kupoteza fahamu.
Akizungumzia
tukio hilo mmiliki wa nyumba hiyo Yasinta Patrick (32) amesema mtu huyo
na wenzake walivamia katika nyumba yake, ambayo ameipangisha kwa
wafanyabiashara wawili wa kutoa na kutuma fedha kwa njia ya mtandao
0 comments :
Post a Comment