.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

Cannavaro: Kwa dozi hii, Simba waje tu uwanjani

 
Wachezaji wa Yanga wakifanya mazoezi kujiandaa na Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.Picha na Mpiga picha wetu 

NAHODHA wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amesema kwa mazoezi ya wiki mbili waliyofanya chini ya kocha Ernest Brandts ana uhakika kikosi chao kipo tayari kupambana na Simba Desemba 21 mwaka huu.
Simba na Yanga zinatarajiwa kupambana siku nne kabla ya sikukuu ya Krismasi katika mchezo wa Nani Mtani Jembe ulioandaliwa na wadhamini wao Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) na kusimamiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Cannavaro aliliambia Mwanaspoti kuwa hadi sasa kikosi chao kipo tayari kwa pambano hilo licha ya baadhi ya wachezaji kuwa katika kikosi cha Kilimanjaro Stars.
“Tunafanya mazoezi mazuri na kocha wetu, tunafanya mazoezi uwanjani, ufukweni na gym, lengo ni kuwa na stamina ya kutosha kuweza kuwahimili wapinzani wetu. Najua tunacheza na Simba siku chache zijazo, sisi tupo fiti sasa kwani tuliwatangulia wiki moja ya mazoezi,” alisema Cannavaro ambaye ni nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Zanzibar.
Nahodha huyo anayecheza nafasi ya beki wa kati, alisema ana imani kila mchezaji wa Yanga aliyeshiriki kikamilifu mazoezi ya timu hiyo yupo tayari kupambana na timu yoyote watakayokutana nayo kuanzia sasa.
Yanga inaendelea na mazoezi yake ya kila siku asubuhi kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam na wakati mwingine huwa wanaenda gym au ufukweni kwa lengo la kuboresha stamina na pumzi kwa wachezaji wake.

Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad