.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

Mishahara Simba yamtesa kocha

 
Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic ameeleza kuwa kuna mambo mengi yanayotakiwa kufanyiwa kazi katika kikosi cha Simba ili timu ifanikiwe na jambo la kwanza aliloona halijakaa sawa ni mishahara ya wachezaji  

BAADA ya kufanya mazoezi kwa wiki nzima, Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic amesema kuna mambo mengi yanayotakiwa kufanyiwa kazi katika kikosi cha Simba ili timu ifanikiwe na jambo la kwanza aliloona halijakaa sawa ni mishahara ya wachezaji na uwajibikaji wao uwanjani.
Logarusic, raia wa Croatia aliiambia Mwanaspoti kuwa wachezaji wengi wa Simba wanalipwa fedha tofauti na kazi au viwango walivyo navyo, hivyo ni lazima uongozi uwe makini na jambo hilo.
Kocha huyo aliyepewa mkataba wa miezi sita kuinoa klabu hiyo, alisema wachezaji wengi wa timu hiyo wanalipwa kiasi kikubwa cha fedha huku wakionyesha uwezo mdogo uwanjani.
“Kuna wachezaji hapa wanalipwa mishahara kama wachezaji wa kulipwa lakini matendo yao ndani na nje ya uwanja ni kama wachezaji wa ridhaa, sasa hili ni tatizo katika timu unayotaka mafanikio ndani ya muda mfupi,” alisema Logarusic mwenye umri wa miaka 51.
Mwanaspoti lilimshuhudia Logarusic akikasirika mara kwa mara alipokuwa akitoa maelekezo kwa wachezaji wakikosea jambo lililomfanya awaite wachezaji wote mara kwa mara na kuwaelekeza jambo la kufanya.
Zoezi lililoonekana kumkwaza zaidi kocha huyo ni lile la wachezaji wawili kushindwa kumtoka beki mmoja na kufunga ambapo mabeki walifanya vizuri kwa kuwazuia washambuliaji na viungo waliopewa jukumu la kufunga.
“Zoezi lile ni dogo tu la kupima uwezo wa mchezaji awe kiungo, beki au mshambuliaji, lakini umeona wengi wameshindwa kufunga kwa kuwa wanafanya mambo kama wachezaji wa ridhaa, wakati wanalipwa kama wachezaji wa kulipwa,” alisema Logarusic.
Hata hivyo, Logarusic aliliambia Mwanaspoti hawezi kuingilia mambo mengi ya wachezaji kwa kuwa wengi wana mikataba ambayo haiwezi kuvunjwa kwa kuwa klabu itaingia gharama kubwa.
“Nitafanya kazi na wachezaji hawa hawa hadi mambo yakapokaa vizuri na kwa uzoefu wangu najua nitafanikiwa kama watanielewa,” alisema Logarusic aliyewahi kuinoa Gor Mahia ya Kenya.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad