.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

KOCHA MKUU WA SIMBA ASEMA ANASUBIRI MIUJIZA


KOCHA Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, amesema ni miujiza tu ndiyo inayoweza kuifanya timu hiyo ichukue ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu kwani mambo yamezidi kuwa magumu ingawa hawakati tamaa na watapambana mpaka mwisho kujua wako nafasi ipi.
Simba ipo nafasi ya nne ikiwa na pointi 32, nne nyuma ya vinara wa ligi hiyo Azam wenye pointi 36 huku Yanga ikiwa ya pili kwa kuwa na pointi 35 sawa na Mbeya City.
Lakini licha ya timu hiyo kuwa nyuma ya wapinzani wao kwa pointi hizo, pia imecheza mechi nyingi zaidi ya Yanga na Azam. Simba imecheza michezo 18 wakati Yanga na Azam zimecheza michezo 16 hivyo zina mechi mbili mkononi.
Timu hiyo imeambulia pointi mbili tu katika mechi zake tatu ilizocheza mikoani na imebakiza mechi mbili za nje ya Dar es Salaam dhidi ya Prisons Machi 3 na Kagera Sugar Machi 30.
Logarusic alisema: “Ligi ni ngumu sana na ukiangalia matokeo yetu ya hivi karibuni yanazidi kutuweka mahali pabaya, hivyo ni muhimu kumuomba Mungu. Tunahitaji miujiza ili tupate nafasi mbili za juu ingawa si jambo rahisi, lakini kwenye soka lolote linaweza kutokea.
“Wapinzani wetu kuna mechi mbili bado hawajacheza ili twende sawa na hujui mechi hizo zitakuaje, kama wakishinda basi ndio tutazidi kupotea, lakini kama watapoteza baadhi ya mechi na sisi tukishinda mechi zetu zinazofuata, tunaweza kujipa matumaini.
“Wachezaji wangu wanatakiwa kupambana hadi dakika ya mwisho na mwisho wa ligi tutajua tuko katika nafasi gani.”
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad