.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

Rais hataidhinisha mamilioni ya wabunge











 Ikulu imesema Rais Jakaya Kikwete hatakubali kuidhinisha kama akipelekewa ombi la kuongeza kiinua mgongo cha wabunge kutoka Sh43 milioni hadi Sh160 milioni.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alisema jana kuwa Rais Kikwete hajapokea maombi hayo huku akipinga maelezo kuwa Serikali ilishayakubali.
Gazeti dada la The Citizen wiki iliyopita, lilimkariri Waziri wa Fedha, Saada Mkuya akisema Serikali ilikuwa imepitisha kupandishwa kwa kiwango cha kiinua mgongo kutoka Sh43 milioni hadi Sh160 milioni baada ya kumaliza kipindi cha miaka mitano.
Waziri huyo alikaririwa akisema kuwa kiwango hicho kilipitishwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na tayari wabunge walishaanza kuchukua fedha hiyo licha ya ukweli kuwa Bunge hili halijamaliza muda wake.
Hata hivyo, Rweyemamu alisema nao wamelisoma suala hilo kwenye magazeti na kwamba halijafika Ofisi ya Rais... “Suala hili halijafika Ofisi ya Rais hata kama litaletwa, `I really doubt if the President will endorse such matter’ (Nina shaka kama Rais ataidhinisha suala hili).”
Serikali kupitia kwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi tayari imekanusha vikali taarifa za kupandishwa kiwango hicho cha malipo kwa wabunge.
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alikanusha kuwapo kwa mapendekezo ya wabunge kulipwa kiasi hicho cha fedha.
“Malipo ya wabunge yanalipwa kwa mujibu wa sheria kwa Kiingereza inaitwa Political Service Retirement Benefits Act (Sheria ya Malipo ya Utumishi kwa Viongozi wa Kisiasa) ni sheria namba 3 ya 1999, kwa hiyo hakuna malipo yoyote yanayoweza kufanyika nje ya sheria hiyo,” alisema Dk Kashililah na kuongeza:
“Sheria inaelekeza kila kitu, kwa kuzingatia uhalisi wa mishahara ya wabunge kwa sasa, malipo yao ya mwisho hayawezi kufikia kiasi cha Sh160 milioni, hata kama mishahara itaongezwa haitaweza kufikia kiwango ambacho kitamwezesha mbunge kulipwa kiasi hicho cha fedha.”
Katibu huyo wa Bunge alisema malipo ya kiinua mgongo kwa wabunge yanakokotolewa kutokana na kiwango chake cha mshahara tu na siyo malipo ya posho za kuendesha shughuli za kibunge
.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad