.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

UONGOZI WA SIMBA WAWEKA WAZI SUALA LA KUMUONGEZEA MKATABA KOCHA WAO

Uongozi wa Klabu ya Simba umeweka wazi kuwa suala la kumuongezea mkataba kocha wake mkuu wa sasa, Zdravko Logarusic limewekwa pembeni kwa kuwa wanasubiri kuona mwelekeo wa timu yao ambayo imekuwa haina matokeo mazuri hivi karibuni.
Loga raia wa Croatia alisaini mkataba wa miezi sita wakati alipotua klabuni hapo mwishoni mwa mwaka jana, ambapo mkataba huo unatarajiwa kufikia tamati Juni mosi, mwaka huu.
Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga, aliweka wazi kuwa matokeo ya timu katika mechi zilizosalia ndiyo yatapa picha uongozi juu ya kuongeza au kutoongeza mkataba huo.
“Mkataba wake unatarajiwa kufikia tamati Juni mosi, mwaka huu tutaendelea naye mpaka mwisho wa ligi, makubaliano yetu ya awali yalikuwa ni kumpa mkataba wa muda mfupi ili kumuangalia na iwapo atafanya vizuri na kuridhisha basi tutamuongezea.
“Lakini suala hilo litaamuliwa mwisho wa ligi kwa wanachama na viongozi kutathmini kile alichokifanya na kama kubaki ama kutobaki ni maamuzi yatakayotolewa hapo baadaye,” alisema Kamwaga.
Simba inashika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu Bara ambapo hivi karibuni iliambulia pointi mbili kati ya 12 ilizotakiwa kuzipata katika mechi nne za ligi hiyo
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad