.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

TIGER WOODS AMPASUA SHABIKI NA KUMTOA DAMU KWENYE MASHINDANO HUKO MIAMI..PICHA NA STORY ZIPO HAPA..

Tiger Wood ambae ni  mcheza golf maarufu duniani , hapo juzi alipatwa na wakati mgumu baada ya kuwapiga mashabiki zake na mpira wa golf mara mbili huku mmoja wa mashabiki hao waliopigwa na mpira alitoka damu na kumfanya apelekwe hospitali. 

Shabiki alietokwa na damu alikua ni mtalii kutoka Ujerumani, Shabiki huyo alikua akifurahi kuangalia mashindano hayo yanayoendelea huko Doral, mjini Florida huko Marekani, alipigwa na mpira huo baada tu ya mchezaji huyo maarufu tiger woods kufungua shot yake yakwanza ambayo ilitua moja kwa moja kwenye kichwa cha shabiki huyo, na kisha kumpasua na damu kuanza kumwagika kutapaka kwenye shati lake jeupe alilokua amelivaa

Tiger woods alimfata na kumuomba msamaha shabiki huyo alisafiri umbali mrefu kwenda kumuona woods akicheza, kwa kumpooza zaidi woods alimpatia shabiki huyo glovealiokua amevaa ikiwa na saini ya woods.

Picha na maelezo yake yote yako chini..
Baada ya kupiga mpira huo, Hapo woods akiwa na mshangao baada kuona mpira huo umemfata shabiki

Shabiki huyo akiwa na furaha baada kumuona Woods anakuja kumpa pole

Shabiki huyo akipewa huduma ya kwanza

Hapo ni baada ya woods kutia saini glove yake na kumpatia shabiki huyo

Shabiki huyo akifurahi sana baada ya kupewa glove hio

Woods akiwa kwenye kiusafiri akiwa na mchumba wake baada ya mchezo huyo

Woods na Mchumba wake wakielekea kwenye boti yao iliotia nanga pembeni ya Miami Beach, ni kawaida ya woods kuja na boti yake kwenye mashindano hayo tangu miaka ya nyuma....





Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad