.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

BOW WOW ABADILI JINA LAKE LA KISANII, sasa KUANZA KUITWA .......

Shad MossMkali wa muziki wa kufokafoka toka Mamtoni, Bow Wow ameamua kufanya mabadiliko makubwa ya jina lililomtambulisha katika medani ya muziki wa kimataifa kipindi hicho akijulikana kama Lil Bow Wow kabla ya kubadili na kuitwa Bow wow na sasa ametangaza rasmi ujio wa jina jipya atakalokuwa akitumia kunako kwa steji na maeneo mengine ya kumuingizia mkate wake wa kila siku.
Habari zilizotapakaa kwenye mitandao mingi wikiendi iliyopita zinaeleza kuwa rapa huyo amewambia mashabiki zake kuwa baada ya tuzo za BET zitakazofanyika Jumapili ya Juni 29 mwaka huu,  jina lake la kisanii litakuwa ‘Shad Moss’ jina alilopewa na wazazi wake.
”’Tangazo : Baada ya Tuzo za BET sitakuwa nikitumia tena jina la Bow Wow! nitatumia  jina langu la halisi ”Shad Moss” tumeweka historia kubwa kama bow wow. Sasa ni muda wa kufungua ukurasa mpya na changamoto. Bow wow haliendani na jinsi nilivyo kwa sasa. Mimi ni baba, mfanyabiashara, mtangazaji, muigizaji na Rapa! Muda wa MR Moss kuchukua hatamu yake” alisema Bow Wow kwenye video fupi aliyoipakia(upload) kwenye ukurasa wake wa instagram.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad