Rapper Fareed Kubanda aka Fid Q amedai kuwa amejaribu kufanya
mazungumzo na viongozi wa mkoa wa Mwanza ili wajaribu kuweka sanamu za
wasanii walionyesha mchango katika mkoa huo.
Akizungumza na kipindi cha Mkasi TV, Fid Q amesema kwa mchango
wanaonyesha wasanii katika nyanja mbalimbali wanahitaji heshima hiyo.
“Juzi nilikuwa Mwanza nikajaribu kukutana na meya, idea ya kumwambia
ni kwamba ili sanaa iweze kukua kwa mfano mimi binafsi nimekuwa
nikiwakilisha mkoa wa Mwanza kwa mwaka wa 15, nastahili status Mwanza,
unakuja pale Mwanza pale garden unakutana na bango kubwa la Fid Q,
sometime inabidi uwape watu idea kwa sababu sisi tupo nyuma ya muda,”
alisema. “Kwahiyo ili tufike inatakiwa tukimbie muda ambao wao
wanatembea, vitu vidogo tu sanaa unakuza hivyo, kuinspire vizazi
vinavyokuja, kwamba ‘okay inabidi nijitume kwa bidii ninaweza nikafika
level za kama Fid Q’, labda unapewa mpaka status unapewa mpaka majumba
ya kumbukumbu,” aliongeza.
0 comments :
Post a Comment