Rapper Shetta amedai kuwa baada ya kutoka kwa video yake mpya ya
Kerewa tayari ameshaanza kupata deal za pesa ambapo DSTV wameshaonyesha
nia ya kufanya kazi na msanii huyo.
Akizungumza na 225 ya XXL ndani ya Clouds FM, Shetta amesema kuwa
tayari wapo kwenye mazungumzo na no na DSTV na hivi karibuni kila kitu
kitakuwa wazi.
“Wakati Diamond ananiambia ‘weka hela Shetta usiogope kuweka hela
kutangaza muziki wako kuwa tofauti na wanamuziki wengine, fanya muziki
wako kufika mbali’, akimaanisha soko la Afrika nikaona kama ananitania
hivi, almost alikuwa ananiambia kama milioni 20 hivi ukiitoa ile hela
ambayo Godfather ninamlipa, nikaona mbona ni pesa nyingi sana. Lakini
nimejaribu kudhubutu, hiki unachokiona ni king’amuzi cha DSTV ni kama
fursa ambayo nimekutana nayo ni deal ambayo ikiwa rasmi zaidi watu
watagundua nini ambacho kimetokea, lakini mpaka hapa tulipofikia ni kama
nusu yake au robo tatu yake. Godfather aliniconnect na watu wa DSTV,
tukafanya makubalianao na makaratasi yapo. Video yangu imepata rotation
kubwa sana, katika station zote ambazo zinaonekana DSTV, na wamenifollow
kwenye akaunti zangu, wananitangazia vitu vyangu kwenye akaunti zao,
kwahiyo hiyo ni deal kwa upande wangu. Thanks to Diamond, thanks to Tale
na watu wote ambao wamenisupport. Kwahiyo sijutii kwa pesa niliyoweka,”
alisema.
0 comments :
Post a Comment