Jaji Thokozile Masipa, akitoa hukumu hiyo mjini Pretoria, pia amempa kifungo cha nje cha miaka mitatu kwa shtaka la kufyatua silaha.
Pistorius amepelekwa moja kwa moja gerezani.
Upande wa mashtaka ulitaka mwanariadha huyo kupewa kifungo cha miaka 10. Upande wa utetezi ulitaka apewe adhabu ya huduma kwa jamii na kifungo cha nyumbani.
Pistorius alikutwa na hatia na kumuua bila kukusudia mpenzi wake, na kufutiwa mashtaka ya mauaji.
0 comments :
Post a Comment