Friday, 9 January 2015

KIPA WA ARSENAL APIGWA FAINI YA PAUNDI 20,000 KWA UVUTAJI WA SIGARA

Mlinda mlango wa kikosi cha kwanza cha washika mtutu wa jiji la London ‘Arsenal’, Wojciech Szczęsny  amepigwa faini ya paundi 20,000 za Uingereza kwa kitendo chake cha kukutwa akivuta sigara muda mfupi baada ya kupoteza mchezo wa ligi kuu dhidi ya Southampton.
Baada ya Wojciech Szczesny kufumwa na kamera za mapaparazi akivuta sigara
Baada ya Wojciech Szczesny kufumwa na kamera za mapaparazi akivuta sigara
Kufuatia kitendo cha mlinda mlango huyo, meneja wa klabu iyo Arsenal Wenger ameamua kumpa adhabu hiyo kuwa fundisho la kufanya atambue uwajibu wake kwenye klabu.

Wojciech Szczęsny akiwa kazini
Wojciech Szczęsny akiwa kazini
Msala kama huo wa uvutaji sigara uliwahi kumkumbuka kiungo wa kimataifa wa klabu iyo, Jack Wilshare pamoja na nahodha wa zamani ‘William Gallas’  ambapo picha zao zilitolewa kwenye vyombo vingi vya habari.
Jack Wilshare
Jack Wilshare akivuta sigara na rafiki zake jijini Las Vegas, Marekani kwenye pool Party Julai mwaka jana

No comments:

Post a Comment