.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

Hii ndo Kauli ya mwisho aliotoa Marehemu Kapteni John Komba kwa Watoto wake

capt Komba
Kifo cha Mbunge wa Mbinga Magharibi na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya taifa CCM kapteni John Komba ambaye amefariki dunia akiwa hospital ya TMJ February 28 kilitanguliwa na kitu ambacho kinadhaniwa kama kilikua ni ishara ya siku yake ya mwisho.
Claudia John Komba ambaye ni mtoto wa 9 kati ya watoto 11 wa marehemu John Komba ameongea na millardayo.com na kuelezea baadhi ya vitu ambavyo kwao imekua kama kauli ya mwisho kutoka kwa Baba yao ambayo aliitoa siku ya sherehe ya kuzaliwa kwake.
Claudia amesema >>>‘Taarifa ilinifikia mida ya saa 9 akasema anajisikia vibaya ambapo wakati yupo njiani akawa anaweweseka sana, tulipofika TMJ hospital walipofanya vipimo walisema ameshafariki’
millardayo.com Kabla ya hapo kulikua na ripoti ya mzee kuugua?
Claudia John Komba: ‘Zilikuwepo baba alikua amekaa ilikua mida ya asubuhi akawa analalamika anajisikia vibaya tukampeleka hospitali, tukagundua sukari imepanda sana na presha imepanda sana, akatolewa akawa anaendelea vizuri’
‘Juzi tarhe 26 feb ilikua siku yangu ya kuzaliwa, akaita watoto wote akasema nataka kufanya birthday sababu birthday nyingi huwa zinanipita nakua nipo nje, akatukusanya watoto wote, aliongea maneno ya mwisho akatusihi watoto tupendane tusiweke  matabaka kwamba huyu mdogo huyu mkubwa alisema yeye hana mkataba na Mungu’.


Share on Google Plus

About Blog Ya Vijana

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad