.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

CHUCHU AJICHORA TATUU YA RAY, RAY AJIBU

KATIKA hali inayoonesha kuna kitu kikubwa kinakuja mbeleni, msanii wa filamu, Chuchu Hans amejichora ‘tatuu’ inayosomeka kwa jina la Ray huku anayedaiwa kuwa mpenzi wake, Vincent Kigosi ‘Ray’ naye akiwa amejichora tatuu inayosomeka kwa jina la Chuchu.
Ray na Chuchu.
Picha ambazo gazeti hili limezinasa zinawaonesha wawili hao wakipigia ‘promo’ uhusiano wao huku wadau wengi wakiyafananisha mapenzi yao na ya njiwa.

Ili kujua undani juu ya jambo hilo, mwandishi wetu aliwatafuta wasanii hao ambapo Chuchu alionekana kukerwa na swali hilo na kujibu kwa ufupi kuwa hataki kusumbuliwa.

“Hivi hamchoki kufuatilia maisha ya watu jamani? Naomba mniache,” alisema Chuchu Hans.
Kwa upande wa Ray, simu yake ya mkononi iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad