.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

Chuji atangaza kustaafu na rekodi

KIUNGO wa Yanga, Athumani Idd ‘Chuji’, amesema kuwa iwe isiwe, lazima astaafu na taji kubwa au ubingwa kwenye timu ya Taifa na hata klabu yake.
Chuji alisema atahakikisha anapata mataji makubwa akiwa na timu hizo ili akistaafu, afanye hivyo akiwa na rekodi mkononi.
“Umri unaenda na itafika wakati nitasema sasa soka basi, lakini cha msingi inafaa mtu kuangalia ni mafanikio gani umepata kwenye kazi yako ya soka na kipi utajivunia zaidi kama mchezaji, hivyo ninataka kuisaidia timu yangu kupata taji kubwa ili siku nikistaafu niwe na rekodi,” alisema.
“Naamini nikiwa na timu ya taifa na hata kwenye kikosi cha Yanga, lazima nijitahidi ili kufanikiwa.”
Kuhusiana na muda wa kustaafu, alisema bado hajafikiria ni wakati gani atastaafu, akisisitiza: “Kwa sasa bado niko fiti na mwenye afya njema.”
Chuji yuko Kenya na kikosi cha Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, kinachoshiriki mechi za Kombe la Chalenji.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad