.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

Kagawa afakamia msosi kupita kiasi

kiungo wa Man United Shinji Kagawa 

KOCHA Mkuu wa Manchester United, David Moyes amefichua kwamba kiungo Shinji Kagawa alikula kupita kiasi na hivyo kuugua hadi kukosa mechi ya juzi Jumamosi dhidi ya Newcastle United kwenye Ligi Kuu England.
Kiungo huyo wa Japan alikula na kufanya tumbo lake kujaa kupita kiasi na kushindwa kupumua baada ya mechi ya kipigo dhidi ya Everton Jumatano iliyopita.
Kagawa aliwahishwa hospitali usiku huo huo baada ya kulalamika kwamba anashindwa kupumua vizuri.
Akizungumza baada ya mchezo wa kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Newcastle United juzi Jumamosi, Moyes alisema, “Shinji alikuwa anaumwa sana baada ya mechi ya Everton na alifanya mazoezi makali Ijumaa, lakini kwa sasa amepata nafuu.
“Ulikuwa ni ugonjwa mbaya. Nadhani alikula kupita kiasi na tumbo lake likajaa, lakini kwa sasa yuko vizuri.”
Kwenye mechi hiyo, Kagawa alitolewa katika dakika 58, lakini alianza kujisikia vibaya wakati akirudi nyumbani kwake Alderley Edge, Cheshire.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad