.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

Kaseja achimba mkwara Yanga

 
KIPA mpya wa Yanga, Juma Kaseja jana alianza rasmi mazoezi na kikosi chake kipya kwa ajili ya maandalizi ya Ligi Kuu Bara na michuano Klabu Bingwa Afrika.
Kipa huyo alitua kwenye mazoezi ya Yanga kwa staili ya kuchimba mkwara akionyesha kwamba yuko tayari kuchapa mzigo na kukabiliana na changamoto zozote.
Kaseja aliyeichezea Simba kwa takriban miaka 10, amejiunga na Yanga kwa mara nyingine na kusaini mkataba wa miaka miwili. Aliwahi kuichezea Yanga mara ya kwanza mwaka 2008.
Alianza rasmi mazoezi na timu hiyo jana Jumatatu kwenye Uwanja wa Boar, Dar es Salaam na alisisitiza kuwa amepona kabisa tatizo la kifundo cha mguu lililokuwa likimsumbua tangu wiki iliyopita na sasa yuko fiti.
Katika mazoezi hayo Kaseja alionekana mchangamfu isivyo kawaida na hakuonyesha ugeni wowote.
Muda mwingi alikuwa akipiga stori na kufurahi na wenzake huku akionyesha hali ya kujiamini.
Akizungumza na Mwanaspoti, Kaseja alisema amefurahi kuanza mazoezi Yanga na amevutiwa na mazoezi hayo licha ya kuwa ni siku yake ya kwanza.
“Lakini jambo la kwanza kubwa ninalowaambia wapenzi wa Yanga, mimi ni mtu wa vitendo na si mzungumzaji nje ya uwanja, pili, ili mambo yaende vizuri nahitaji sana sapoti ya mashabiki, viongozi na wachezaji wenzangu lakini tatu wafahamu kuwa mimi kama kipa wao siko tayari kuwaangusha ila wakubali kuwa mpira una mambo matatu ambayo ni kushinda, sare na kufungwa,”alisema baada ya kuulizwa ni namna gani ataweza kukabiliana na changamoto za mashabiki ambao wamekuwa na tabia ya kulaumu makipa wanapofungwa.
Aliongez: 'Waone kuwa mpira ni kazi ya watu kama zilivyo kazi nyingine,nilikuwa Simba na sasa niko Yanga lakini eti kwa sababu zamani nilikuwa kule nitashindwa kufanya kazi yangu si kweli,wajue kuwa,upenzi upo hata Ulaya lakini makipa wao wanapofungwa inakuwa sehemu ya mchezo na siyo kuwalaumu na hakuna anayependa kufungwa aharibu kazi yake,”alisema Kaseja.
Akizungumzia mazingira aliyoyakuta jana baada ya kuanza kazi hasa kunolewa na kocha mpya kwake, Razack Siwa kipa huyo alisema: “Nimefanya na kocha, Siwa nafikiri ni mzuri ingawa kwa sasa ni mapema mno kuzungumzia tofauti na yule aliyekuwa ananifundisha Simba, James Kisaka.”
Siwa alisema: “Kaseja ni kipa mzuri na nafikiri ataisaidia timu, tumeanza naye leo (jana) anafanya vizuri.”
Kocha mku wa Yanga, Ernest Brandts alisena: “Kaseja ni kipa mzuri kama unavyojua Yanga, inapenda kuwa na wachezaji wazuri na ndiyo maana yupo hapa.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad