Hii imetokea huko Ufarasa baada ya John Dowling (58) na mwanae Rob (23) kuanza kushindana kuserereka kwenye barafu, mchezo ambao upendwa sana nchini Ufaransa, Baba huyo na mwanae walitumia kiwanja cha barafu ambacho kilikua kinaandaliwa kwa ajili ya mashindano siku inayofata, huku ikiwa imewekwa mageti special ili watu wasipite kwa kuwa uwanja ulikiua kwenye maandalizi.
| Hapo ndipo alipo anguka na kujigonga kwenye Geti hilo la Chuma |
Mtoto huyo aliweza kumpita baba yake, huku baba huyo akijaribu kuongeza mwendo ili amfikie mwanae kwa bahati mbaya akatereza vibaya na kuanguka na kujigonga kwenye geti na kumfanya damu nyingi kuanza kumtoka kichani kwake.
| Akiwa anaangaliwa huku wakiwa wanasubiri usafiri kuja kumchukua kumpeleka hospitalini |
"Baada ya baba kuanguka nilijua kaumia na alianza kupiga makelele sana, nikajua ameumia vibaya ikanibidi nimsaidie kumtoa, alivyopelekwa Hospitali nilibaki nafikiria nikikumbuka kilichomtokea Michael Schumacher, sikujua kama atakufa au atapona, ila nikashangaa baada ya siku tatu amepona na kurudi kwenye kutereza tena kwa spidi." alisema mwanae Rob
| Baba huyo akiwa anapelekwa Hospitali ambapo alitibiwa kwa siku tatu na kuruhusiwa kutoka |
ANGALIA VIDEO HIO HAPA...
0 comments :
Post a Comment