Juhudi za kimataifa zinaendelea kutafuta ndege ya
shirika la ndege la Malaysia iyokuwa ikielekea Beijing nchini China na
kupotea baharini ikiwa na abiria 239.
Ndege hiyo iliyopotea aina Boeing 777 ilkuwa na abiria wapatao 239 pamoja na wafanyakazi wa ndegeAsia ya Kusini Mashariki imeongeza nguvu katika juhudi hizo za kutafuta ndege hiyo iliyopotelea katika eno la bahari la Malaysia na Vietnam .
Shirika la ndege la Malaysia limesema ndege hiyo namba MN370 ilipotea majira ya saa 8:40 kwa saa Malaysia siku ya Ijumaa baada ya kuondoa Kuala Lumpur.
Jeshi la Malaysia limesema kikosi cha pili cha helikopta na Meli kimetumwa kwenye eneo la tukio lakini hata hivyo hakuna chochote kilichoonekana katika hatua za awali za utafutaji wa ndege hiyo.
Ndege hiyo ilitarajiwa kuwasili Beijing China majira ya saa 12:30 kwa saa za Malaysia.
Waziri wa Usafiri wa Malaysia amesema hakuna taarifa za zozote za kuonekana kwa mabaki ya ndege hiyo.
"Tunafanya kila linalowezekana ndani ya uwezo wetu kujua ndege hiyo ilipo," Hishammuddin Hussein amewaambia waandishi wa habari katika mji Kuala Lumpur
hUKU HABARI ZILIZOFIKA ZINA SEMA
Wakuu wa Vietnam wanasema michirizi miwili mikubwa
ya mafuta imeonekana katika bahari nje ya mwambao wa kusini wa nchi
hiyo, huku msako unaendelea kutafuta ndege ya Shirika la Ndege la
Malaysia iliyotoweka Jumamosi asubuhi.
Inasemekana michirizi hiyo miwili sambamba ina urefu wa kama kilomita 15 hadi 20.Ndege na meli kutoka nchi kadha zimekuwa zikifanya msako katika eneo la bahari baina ya Vietnam na Malaysia.
Usiku ulipoingia ndege hiyo ya aina ya Boeing 777 ilikuwa bado haikuonekana - ndege ilipoteza mawasiliano na waongozi wa radar saa mbili baada ya kuanza safari.
Ilikuwa imebeba abiria na wafanyakazi wa ndege 239.
Source. BBC NEWS
0 comments :
Post a Comment