.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

IRENE PAUL: "STEVE NYERERE ANAWEKA MAKUNDI BONGO MUVI.''


UWEZI kuamini! Staa na mtayarishaji wa filamu za Kibongo, Irene Paul amejitoa mhanga na kuanika uozo wa Kundi la Bongo Movie Unity bila woga baada ya kusema halina faida yoyote kwa wasanii wanaounda kundi zaidi ya kuwanufaisha viongozi wake ambao wanalitumia kwa masilahi yao binafsi.

Akiweka woga pembeni tena bila ya kupepesa macho, Irene alisema Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengele ‘Steve Nyerere’ hana sifa za kuwa kiongozi wa wasanii.

“Nyumba ni baba mwenye busara kwa familia yake na anayemudu kuongoza familia yake, lakini mnakuwaje na kiongozi anayegawa watu kama Steve!

“Anaweza kukununia bila hata sababu, hayo na mengine ya ufisadi wa michango mbalimbali siwezi kuyaongelea, lakini ukweli Bongo Movie haina kiongozi,”anasema Irene.

Jitihada za kumtafuta Steve Nyerere kujibu tuhuma hizi hazikuzaa matunda baada ya kutopokea simu pamoja na kwamba ilikuwa ikiita.

Hata baada ya kupigiwa zaidi ya mara nne, Steve hakupokea simu na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno (sms) hakujibu.

Steven Nyerere amejiuzuru Uongozi unaweza kusoma BONYEZA HAPA


Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad