.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

"Nilivamiwa na staa Aisha bui na mabaunsa ambao walivunja ofisi pamoja na kuchukua ‘laptop’ na fedha." asema Ngeze


Staa wa sinema za Kibongo, Aisha Bui akiwaka kwa mmoja wa wahusika wa ofisi za kusambaza filamu za Yuneda, Mbagala.
 Staa wa sinema za Kibongo, Aisha Bui amezua timbwili la kufa mtu katika ofisi za kusambaza filamu za Yuneda zilizopo Mbagala jijini Dar baada ya wasambazi hao kushindwa kumlipa kwa wakati. Mtiti huo ulioshuhudiwa na wanahabari wetu ulijiri wikiendi iliyopita, maeneo hayo ya Mbagala ambapo Aisha aliongozana na shemeji yake katika ofisi hizo na kuibua tafrani kubwa iliyokusanya kadamnasi na kufunga mtaa kwa muda.
Aisha Bui mara baada ya kuvunja kioo cha mlango.

Kwa mujibu wa Aisha, amekuwa akitimba kwenye ofisi hizo mara kwa mara akiomba alipwe chake lakini amekuwa akipigwa kalenda tangu Aprili, mwaka huu. Aisha alilifungukia Ijumaa Wikienda kwamba, kuna siku mkurugenzi wa kampuni hiyo aitwaye Ngeze alimwita ofisini kwake ili kumlipa lakini alipofika alimpa kiasi cha shilingi milioni mbili na nusu, jambo ambalo lilikuwa kinyume na makubaliano.

Aisha Bui akiwa na jiwe lililotumika kuvunjia mlango wa kioo wa ofisi hizo.

“Filamu yenyewe nimeigiza kabla sijajifungua hadi mtoto wangu sasa ana miezi sita. Kama mtu ndiyo unategemea fedha za filamu yako ndiyo uendeshee maisha, halafu mtu halipi, sasa utaishije?
 Staa huyo alisema alikuwa akimpigia simu mara kwa mara mwisho mkurugenzi huyo aliamua ‘kum-block’ kwenye simu hivyo akawa amekosa mawasiliano naye.

Wananchi wakishuhudia varangati lililoanzishwa na Aisha Bui.

Aisha alipofika ofisini hapo alishikwa na ghadhabu baada mhasibu wa kampuni hiyo kumwambia hakuwa na namba ya bosi wake wakati alijua akifika tu angepewa fedha hizo hivyo akashikana naye mashati na kuanza kuzipiga ambapo Aisha alisukumwa akadondoka pwaa!
Kitendo cha kusukumwa, kilimpandisha hasira Aisha na kuamua kuchukua jiwe ambalo lilishindwa kufungua mlango hivyo alichukua nondo na kuvunja mlango huo ambapo wafanyakazi walijifungia kwa ndani ili kumzuia asiingie ndani.

Aisha Bui akiondoka eneo la tukio.

Wanahabari wetu walipomfuata  Ngeze kujua kulikoni kumtia mbaroni Aisha alisema alivamiwa na staa huyo na mabaunsa ambao walivunja ofisi pamoja na kushukua ‘laptop’ na fedha.

Hadi gazeti hili linaondoka eneo hilo, Aisha na shemeji yake walikuwa bado wameshikiliwa na Polisi wa Kituo cha Maturubai, Mbagala.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad