Wayne Rooney alishangilia goli lake kwa style ya mchezo wa Boxing, ikijaribu kuonesha jinsi taarifa ya kupigwa kwake knock-Out nyumbani kwake na mchezaji mwezake wa wazamani.
Picha zilizosamba juzi usiku zikimuonyesha Mchezaji huyo wa Manchester United ametupwa chini wakiwa wanacheza mchezo wa ngumi katika nyumba yake yenye thamani ya paundi million 3.5 akiwa na beki wa stoke city Phil Bardsley.
Baada ya kufunga goli la tatu dhidi ya Tottenham Hotspur hapo jana, Rooney alishangilia kwa kurusha ngumi hewani kabla ya kuanguka chini
Wayne Rooney akishangilia goli kwa style ya mchezo wa boxing, akiwa ana ashilia alivyo pigwa Knock-Out na mchezaji mwezake wazamani
Rooney akijitupa chini akiiga picha zilizoenea akiwa amepigwa, Ashley Young akicheka nyuma
Picha zilizoonekana juzi usiku zikimuonesha mshambuliaji huyo akiwa amevaa gloves za boxing huku yeye na Bardsley ( Mchezaji wazamani wa Man United) wakaanza kupambana.
Kuna uwezakano mshambuliaji huyo akazungumziwa na chiefs wa Man Utd, ambao inasemekana wanamlipa paundi 300,000 kwa wiki, Rooney anaonekana analichukulia jambo hilo kama mchezo tu.
Baada ya kufunga goli la Tatu hapo jana huko jiji Manchester, Rooney alikimbilia kwa mashabiki kabla ya kurusha ngumi hewa. kisha akafumba macho kabla ya kujitupa chini.
Pambano la ngumi lililotokea jiko kwa Rooney, Chanzo kiliiambia mtandao wa The Sun "Wayne alifanya kila mtu apate wasiwasi alipo anguka chini. Alijitupa chini huku macho yake akiwa amefumba, hatingishi kitu."
"Watu waliogopa, aligongesha kichwa chini na kujiumuza kidogo. Kila mtu akajua ili kuwa kitu cha kijinga kufanya."
Inasemekana tukio lilitokea siku moja baada ya United kupigwa na Swansea, huku mke wake Coleen na watoto wao Kai na Klay walikuwa mapumziko huko Barbados
Clip io yenye urefu wa dakika moja , ikionesha watu wawili wakirushiana ngumi huku marafiki wakicheka na kutaniana.
Tukio hilo linaweza muweka Rooney katika wakati mgumu kutegemea maswali kutoka kwa Manager wa Manchester United Louis van Gaal.
Van Gaal anaonekana ajaridhishwa na mshambuliaji huyo kujihusisha na michezo hatari akiwa ana mechi na mazoezi karibuni.
Hii ni kutokana na wachezaji wengi kuwa na kipengele kwenye mkataba wao kinacho wakataza kujihusisha na michezo hatari ili kujizui kupata majeraha.
Bardsley ni mchezaji wazamani wa Manchester United, wawili hao walicheza pamoja kabla ya Mscotland huyo kuondoka na kusign Sunderland mwaka 2008
Kisha kuamia Stoke City mwaka jana, huku mke wake Tanya amepata umaarufu baada ya kuanza kuonekana katika kipindi cha The Real Housewives of Cheshire kama starring.
Ukiongelea miaka saba iliopita, Rooney alisema mazoezi ya boxing akiwa mtoto yalisaidia maisha yake ya mpira."
'Nathani mazoezi ya boxing yalinisaidia kujiendeleza kama mchezaji, yalisaidia zaidi mimi kuweza kuwika ligi kuu nikiwa mdogo.' alisema rooney mwaka 2008.
'Nilihitaji nguvu yaziada kutoka kwenye mazoezi ya boxing na nilipata, ikawa rahisi kucheza sana, imenisaidia hata jinsi uchezaji wangu ulivyo sasa.
'Maisha yangu yote - tangu nikiwa na miaka 6, 7 na 8 - kukiwa na mapambano makubwa kwenye Tv, nilikuwa nakesha na baba kuangalia.
'Napenda boxing na nilisha fanya mazoezi nikiwa mdogo, ndo mchezo ambao nilijihusisha nao utotoni.
'Nilikuwa nafanya mazoezi ya boxing na mpira kwa nyakati moja nikiwa na miaka 15. Ila Everton ambao nilikuwa nao wakati huo, waliniambia nilitakiwa kuzingatia kimoja na nikachagua mpira.'
Wajanja Tukutane huku tuzungumzie kila kitu.....
Follow Twitter CLICK HERE
Follow Instagram CLICK HERE
0 comments :
Post a Comment