.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

Ngassa ampeleka Shomari Kapombe Yanga


BEKI wa zamani wa Simba, Shomari Kapombe aliyekuwa anaichezea klabu ya As Cannes ya Ufaransa inayoshiriki Ligi Daraja la Nne juzi Jumapili aliongozana na Mrisho Ngassa mguu kwa mguu kuiona Azam FC ikicheza na Ferroviario ya Msumbiji.
Ingawa haijulikana walitokea, lakini Kapombe anayewindwa na Yanga, aliingia kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi nje kidogo ya Dar es Salaam akiwa na Ngassa kuangalia pambano la Kombe la Shirikisho Afrika baina ya Azam FC na Ferroviario.
Beki huyo mara baada ya kuingia uwanjani hapo, walikaa jukwaani na kufuatilia mechi hiyo kwa makini iliyomalizika kwa Azam FC kushinda bao 1-0 na baadaye wakaondoka pamoja.
Tofauti na hao, wachezaji wengine wa Yanga waliofika uwanjani hapo kwa ni Emmanuel Okwi, Hamis Kiiza na kipa Juma Kaseja .
Mara baada ya mechi hiyo kumalizika, Kapombe aliongoza na kiungo huyo na kuondoka zao muda mfupi baada ya  Okwi na Kaseja kuondoka.
Kapombe yuko nchini  baada ya kugoma kurudi Ufaransa akishinikiza kulipwa malimbiko ya mishahara na stahiki zake.
Habari za ndani zinasema kuwa Kapombe amekuwa karibu na viongozi wa Yanga na kuna uhakika mkubwa msimu ujao anaweza kuvaa jezi za njano na kijani.
Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad