.

.

SHOP HERE

News
Loading...

.

.

.

shop now

List mpya ya Klabu 20 Tajiri Duniani





Takwimu mpya za klabu klabu tajiri 20 barani Ulaya zinaonyesha kuwa klabu tano za Ligi Kuu England zimepenya kwenye orodha ya kumi bora.

Orodha hiyo mpya iliyoandaliwa na wataalamu wa masoko kutoka Shule Kuu ya Biashara ya London kwa mara ya kwanzawamefanya uchunguzi na kubaini klabu tajiri Ulaya.

Katika orodha hiyo, Real Madrid imeendelea kukaa kileleni, Manchester United inafuata kwa karibu.

Lakini, Manchester City ambayo imeendelea kujikusanyia rasilimali kutokana na uwekezaji wa matajiri wa Kiarabu imepanda hadi nafasi ya nne, ikitanguliwa na Barcelona.

Man City ilinunuliwa na Sheikh Mansour bin Zayed Al Nahyan mnamo mwaka 2008 na tangu wakati huo imeshuhudia kupanda kwa thamani yake soko kwa asilimia 94 kwa miaka mitano iliyopita.

Klabu za England
Chelsea, Arsenal na Liverpool zimeshika nafasi za sita, saba na nane, mbele ya Juventus, Borussia Dortmund na Paris Saint Germain. Tottenham, Newcastle na West Ham, pia zimeingia kwenye orodha ya 20 bora.

Ni klabu tano pekee Ulaya ambazo zinaingia kwenye orodha ya mabilionea, zikiwamo Bayern Munich iliyoko nafasi ya tano na Chelsea inayokamata nafasi sita.

Utafiti zaidi wa wasomi hao umeonyesha kuwa, Man United ina mashabiki wengi duniani, inafuatiwa kwa karibu na Liverpool, Real Madrid, Chelsea na Barcelona.

Wataalamu hao wanasisitiza kuwa mafanikio hayo ya klabu yametokana na uwekezaji, kuuza majina yao, idadi ya mashabiki na idadi ya nyota walio nao.

Mtaalamu Jacques de Cock kutoka shule hiyo ya biashara ya London alisema "Majina na bidhaa kama jezi za klabu ni mambo muhimu katika kuziwezesha klabu kupiga hatua hasa Uingereza na Hispania, ambako klabu zao zimetawala

20 - GALATASARAY { Pauni 187 mil }

19 - WEST HAM UNITED { Pauni 196 mil }

The Olympic Stadium in London
 Uwanja mpya wa West Ham wanategemea kuhamia msimu ujao

18 - NEWCASTLE UNITED { Pauni 222 mil }
 Newcastle United owner Mike Ashley and wife Linda Ashley watch from the stands alongside Newcastle United chief executive Lee Charnley 
 Mmiliki wa Newcastle United Mike Ashley

17 - NAPOLI - {Pauni 224 mil }

16 - ATLETICO MADRID { Pauni 277 mil}

15 - INTER MILAN { Pauni 279  mil}

14 - FC SCHALKE 04 { Pauni 363 mil}

13 - TOTTENHAM { Pauni 381 mil}

12 -PARIS ST GERMAIN { Pauni 403 mil}

11 - BORUSSIA DORTMUND { Pauni 445 mil}

10 - AC MILAN { Pauni 492 mil }

09 - JUVENTUS { Pauni 531 mil }

08 - LIVERPOOL { Pauni 624 mil }

07 - ARSENAL {Pauni 832 mil }

6 - CHELSEA { Pauni 870 mil }

5 - BAYERN MUNICH { 1.492 bilioni }

4 - MANCHESTER CITY { 2 bilioni }
 
Mmiliki wa Man City: Sheikh Mansour bin Zayed Al Nahyan
  
3 - BARCELONA - {2.007}
 
2 - MANCHESTER UNITED - { 2.05 bilioni }

1 - REAL MADRID { 2.07 Bilioni }

Share on Google Plus

About feisal pinto

Computer Application Student, Author, Short Stories Writer, Business Proposal Writer, Presenter and Application Builder. Email feisalpinto4@gmail.com for complains and business only.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

ad